Robin van Persie ameonekana akitembea huku na kule katika mitaa ya mji wa Rome nchini Italia.
Hali hiyo imeonekana kuzua gumzo kwamba huenda mshambuliaji huyo anaweza
kutua AS Roma.
Van
Persie alikuwa na mkewe Bouchra akipiga mitaa hali iliyosababisha
baadhi ya vyombo vya habari kuamini huenda atahamia Italia.
Mkali huyo wa mabao kutoka Uholanzi amekuwa na msimu wa kubahatisha Manchester United, inakuwa ni
lahisi sana kwake kuondoka.
Tayari
kumekuwa na taarifa kwamba Roma walikuwa na mpango wa kumnasa Mholanzi
huyo mwenye miaka 31. Hata hivyo, hadi sasa hakuna uhakika kuhusiana na
hilo.
Post a Comment