Meneja wa msanii huyo, Babu Tale, awali
aliulizwa na gazeti hili juu ya kinachoendelea kuhusiana na vijana hao
waliotimuliwa shule Aprili mwaka huu kwa kutolipiwa ada, lakini
akionekana kupatwa na jazba, alisema wanasikitishwa na jinsi wazazi wa
watoto hao wanavyokiuka makubaliano, hivyo wao hawataki tena kusema
lolote kwa sasa.
“Kama wao wanadhani kwa kwenda kwenye
media (vyombo vya habari) ndiyo watoto wao watasomeshwa, basi na waende
hukohuko watasomeshewa watoto wao,” alisema Tale aliyeonekana
kukasirishwa na mwendelezo wa habari hiyo.
Tale alitoa kauli hiyo kufuatia mmoja wa
wazazi hao wa watoto Hillary na Hamis, kudai kuwa hakuna maendeleo
yoyote ya kulipiwa ada kwa vijana wao, kwani ingawa waliambiwa mambo
yangekuwa sawa baada ya siku chache, lakini danadana zinaendelea.
Mwanasheria mmoja maarufu nchini
aliyeomba hifadhi ya jina lake, aliliambia gazeti hili kuwa endapo
wazazi wa vijana hao wataamua, sheria zinawaruhusu kumpeleka mahakamani
msanii huyo kwa kukiuka mkataba, hata kama haukuandikwa.
“Makubaliano ya mdomo ni mkataba
unaotambuliwa kisheria, mradi tu wazazi waweze kuthibitisha, tena kwa
hili, inaonyesha siyo tu mkataba, bali inaonyesha Diamond hakufanya
hivyo kwa mapenzi yake kwa watoto, bali baada ya wao kumfanyia kitu,
aliwapeleka shule kuonyesha u-siriazi aliokuwa nao juu ya ahadi hiyo,”
alisema mwanasheria huyo.
Januari mwaka jana, Diamond aliendesha
shindano kwa watoto la kucheza mtindo wa Ngololo na kuahidi zawadi kwa
washindi katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar. Vijana hao
walioshinda, walipewa ofa ya kusomeshwa katika shule hiyo hadi kumaliza
elimu yao ya msingi, lakini tangu wapelekwe hawajawahi kulipiwa ada.
Post a Comment