Hapo kati mamsapu aliniletea sana za
kuleta na siku moja akanitamkia wazi kuwa amechoka kuishi na mimi
(baadae aliomba msamaha akasema alipandwa na hasira). Kipindi
tulichochuniana nikakutana na kadem fulani na nikawa nimeamua mamsap
akisepa tu, navuta jumla hako kadada.(ni kadada kwa sababukiumri
nakazidi sana halafu ni kipotabo). Sasa wife hakusepa wala nini na mimi
nikawa nimekolea nje mpaka nimepangishia chumba na gheto
nimelikamilisha. Wife alikuja futa kauli zake za kuondoka hazingui tena
na kawa mpole na mwenye heshima mpaka naona aibu kuendelea na nyumba
ndogo. Wife Sitaki kumwacha na nyumba ndogo naonahuruma kummwaga kwa
sababu yaani kakolea kishenzi. Sidhani kama atamwamini mwanaume mwingine
Mimi nikimtosa. Naogopa kumwambia wife nataka oa mke wa pili kwa sababu
atasepa, japo ningewamudu na napenda wake wawili. Kitu kingine mamsap
hapendi kujishughulisha na utafutaji hela wakati hii nyumba ndogo
inajituma kwenye utafutaji kishenzi (mchaga), mara kadhaa ashanikwamua kwenye vishida vya lakilaki hizi. Sasa nipo kwenye dilemma!!
Post a Comment