Featured

    Featured Posts

Mashaidi 15 Kutoa Ushahidi Kesi ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania, Johnson Minja.



Serikali imeandaa zaidi ya mashahidi 15 kwa ajili ya kutoa ushahidi kwenye kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania, Johnson Minja.
 
Minja alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Dodoma jana na kusomewa maelezo ya awali ya kesi inayomkabili. Alikana mashtaka yote mawili ya uchochezi mbele ya Hakimu Rhoda Ngimilanga.
 
Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Paul Kadushi alidai kuwa Septemba 6, 2014, mshtakiwa akiwa katika Chuo cha Mipango kilichopo Kata ya Miuji, Manispaa ya Dodoma, alitoa kauli zilizochochea kutendeka kwa kitendo cha jinai kinyume na sheria.
 
Katika kosa la pili siku hiyohiyo, mshtakiwa alitenda kosa kwa kuzuia ukusanyaji wa kodi kwa kuwachochea wafanyabiashara nchini kutotumia mashine za kielektroniki za kukusanya kodi (EFDs).
 
Hata hivyo, Minja alikubali baadhi ya maelezo yaliyotolewa baada ya kusomewa na wakili huyo wa Serikali.
 
Alikubali mahakamani kuwa anatambua kuwapo na sheria ya matumizi ya mashine za kielektroniki kwa ajili ya kukusanyia kodi, sheria ya kukusanya kodi na utambulisho wake uliotolewa mahakamani.
 
“Ni kweli kuwa Septemba 6 mwaka jana, tulifanya mkutano katika Chuo cha Mipango kwa lengo la kuwapa wafanyabiashara mrejesho wa maendeleo ya mazungumzo yetu na TRA kuhusu matumizi ya EFD ili kuiongezea Serikali mapato bila kuua uchumi wa nchi na mfanyabiashara mwenyewe,”  Minja.
 
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 8 na itasikilizwa kwa siku tatu mfululizo hadi Juni 10.

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

.....


Powered by Blogger.

Translate

Total Pageviews

Copyright © HABARI ZA LEO | Designed By Code Nirvana