Featured

    Featured Posts

Kama si urais ningekuwa mwanamuziki-JK Rais Jakaya Kikwete (kulia) akiwa na Naseeb Abdul 'Diamond Platnum


Rais Jakaya Kikwete (kulia) akiwa na Naseeb Abdul 'Diamond Platnum
Rais Jakaya Kikwete (kulia) akiwa na Naseeb Abdul 'Diamond Platnum' alipotembelea Ikulu jijini Dar es Salaam
RAIS Jakaya Kikwete, ametoa mpya. Anasema kama asingekuwa Rais, huenda angekuwa mwanamziki mashuhuri wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Fleva, kutokana na kipaji alichonacho.
Akihutubia sherehe za wafanyakazi jijini Mwanza leo, Kikwete alianza kwa kuimba kibwagizo cha wimbo wa “mimi msafiri bado niko njiani” ulioimbwa na mmoja wa wanamziki wa zamani, akisema matatizo ya wafanyakazi hao ni sawa na msafiri.
Ni katika kibwagizo hicho, Kikwete alijisifu akisema “kama sio urais pengine nami ngekuwa mwanamziki wa Bongo Fleva…maana sauti nzuri ninayo na niweza kuimba, japo nisingekuwa maarufu kuwapita akina Ali Kiba na Diamond (Naseeb Abdul).”
Kauli yake iliibua vicheko uwanjani hapo, kuanzia viongozi waliokuwa wameketi naye meza kuu hadi kwa maelfu ya wafanyakazi waliohudhuria hafla hiyo.
Licha ya Rais kufanya mzaha, lakini amekuwa mdau mkubwa wa sanaa ya mziki wa kale na sasa, jambo ambalo amelipa msukumo mkubwa wakati wa uongozi wake kwa kuwawezesha wasanii.
-chanzo:Mwanahalisi online

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

.....


Powered by Blogger.

Translate

Total Pageviews

Copyright © HABARI ZA LEO | Designed By Code Nirvana