Chama
cha ACT-Wazalendo kintarajia kutoa fursa kwa watangaza nia wa nafasi
mbalimbali katika mkutano wake wa kitaifa utakaofanyika tarehe 13 mwezi
huu.
Hatua
hiyo inafuatia joto la urais kuanza kupanda ndani ya vyama mbalimbali
vya kisiasa nchini kikiwemo chama tawala cha Mapinduzi (CCM).
Kwa
mujibu wa Katibu Mawasiliano na Uenezi wa Chama wa ACT –wazalendo
Sabini Richard amesema chama hicho kimejipanga kushiriki katika
uchaguzi mkuu hivyo kutakuwa na mkutano mkuu utakaofanyika mkoani
Tabora.
Katika
mkutano huo watahuisha azimio la Arusha lengo likiwa ni kudumisha
misingi ya amani, udugu na uzalendo kwa lengo la kuwaunganisha
watanzania pamoja na kuenzi harakati za ukombozi barani Afrika.
Post a Comment