Mwisho wa
jeuri? Mzazi mwenza wa staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa
Mitego’, Siwema Edson anadaiwa kumwangukia mwanamuziki huyo ili
warudiane walee mtoto wao.
Habari kutoka chanzo cha kuaminika
ambacho ni ndugu wa Siwema kilieleza kuwa, pamoja na maneno ya shombo
aliyommwagia Nay wakati wanaachana, mrembo huyo kwa sasa ameweka silaha
chini akiomba wawe kama zamani.
Kilidai kwamba hivi karibuni, mmoja wa
dada wa Siwema (jina linahifadhiwa) amekuwa akimpigia simu Nay akimuomba
arudishe moyo wake kwa Siwema, kwani tangu aachane naye mambo yamekuwa
yakienda kombo ikiwemo ule msala wa kesi inayoendelea mahakamani ya
kujipatia mali isivyo kihalali.
Ney wa mitego , Siwema Edson wakiwa na mtoto wao.
Baada ya kumwagiwa ubuyu huo, Ijumaa Wikienda lilituma
kijumbe kumfikishia Nay ombi hilo la Siwema ambapo alikuwa na haya ya
kusema: “Kweli nimepokea simu za msamaha. Nimemsamehe lakini siwezi
kurudiana naye.”
Kwa upande wake mama Nay alisema yeye ndiye alikuwa mtetezi wake lakini kwa sasa hataki kusikia ishu hiyo
Post a Comment