Featured

    Featured Posts

SAMATTA HUYOOOOO! BARANI UROPA...



SASA hakuna jinsi! lazima Mbwana Samatta akacheze soka la kulipwa barani ulaya! 
Hivi ndivyo unaweza kusema baada ya meneja wa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Tanzania na TP Mazembe ya DR Congo, Jamal Kasongo kusema wameshakaa na mmiliki wa Mazembe, Moise Katumbi kujadili juu ya kuuzwa kwa Samatta.
"Katumbi anafahamu wazi kuwa Samatta kabikisha mwaka mmoja, aliniita juzi juzi tu kujadili suala la mtoto (Mbwana Samatta). Muda mpekee kwa Katumbi kutengeneza pesa ni majira ya kiangazi mwaka huu au majira ya baridi mwezi januari mwakani, akishindwa hapo mwezi wa nne mwakani Mbwana atakuwa mchezaji huru, ataondoka klabuni bure, Katumbi (Moise) hawezi kukubali hilo".
"Kutokana na mazingira haya, suala la Samatta kwenda ulaya majira ya kiangazi mwaka huu halina ubishi, lazima aondoke".
Pia Kasongo amesema Samatta alishindwa kujiunga na CSK Moscow dirisha dogo la usajili mwezi januari mwaka huu kutokana na kupata majeraha siku moja kabla ya kucheza mechi ya kirafiki ambayo maamuzi yangetoka moja kwa moja.
"Katika siku tatu alizofanya majaribio CSK Moscow alicheza vizuri mno, alifunga magoli matatu, siku ya kucheza mechi ya kirafiki aliumia kifundo cha mguu na hakutumika katika mchezo huo ambao ungetoa majibu. CSK wametoa muda mwingi mrefu wa majira ya kiangazi kwa Mbwana (Samatta)".

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

.....


Powered by Blogger.

Translate

Total Pageviews

Copyright © HABARI ZA LEO | Designed By Code Nirvana