Jinsi ya kuchagua jinsia ya mtoto
"Nina kukubali uwezo wako kiushauri na
kiuzoefu,Umejaliwa!!..Mimi ni kijana wa kiume mwenye umri wa miaka
27,nina mchumba wangu na tuko kwenye harakati za kufunga ndoa.
Tatizo langu ni hili: Napenda sana first born
wangu awe wa kike;[tei tei.....],na ninasikia kuna namna fulani ya
kuweza kupanga jinsia ya mtoto japo ni kwa majaliwa ya mungu.
NIFANYEJE???? Naomba unisaidie jamanii!! Wako B.Z"
*****************************
Dinah anasema: Ahsante, Nashukuru sana.
Ni kweli kuna namna ya kuchagua Jinsia ya mtoto kabla Mimba haijatungwa
lakini bado haijathibitishwa Kisayansi/Kitaalam.
Kupata mtoto wa Kike sio ngumu sana kama
ilivyo kwa mtoto wa kiume + inategemea zaidi kwenye uwingi wa jinsia
hiyo upande wako(familia ya mwanaume).
Mbegu zinazosababisha mtoto wa kike
"hutembea" taratibu kuelekea kwenye Yai na huishi kwa masaa
72-Wiki....hivyo wewe na mkeo hamtahitaji kusubiri "tarehe" maalum.
Kama kwenu au kwa baba mdogo/ mkubwa kuna wanawake wengi basi unaweza ukafanikiwa kupata Binti bila taabu kabisa.
Ila epuka kufanya mapenzi tarehe ambazo mkeo ajae anakaribia kupevusha Yai....fanya mapenzi baada ya hedhi na wiki mbili baadae.
Mbegu zinazosababisha mtoto wa kiume
zipo "faster" na hufa haraka, hivyo kama unataka mtoto wa kiume inabidi
kutegea "tarehe" maalum ili Mbegu iliwahi yai likiwa njiani...
Japokuwa suala la mtoto wa kiume
linategemea zaidi upande wa Mwanamke, ikiwa kwako kuna wanaume wengi au
idadi sawa na wanawake, urahisi wa kupata mtoto wa kiume ni kubwa.
Sehemu ya maelezo yangu ni kutokana na
uzoefu wangu binafsi, tulipotaka mtoto wa kwanza awe wa Kiume tulikuwa
tunafanya kwa kufuata "tarehe" maalum + mikao maalum(hakuna kifo cha
mende wala vijiko)!!
Mtoto wetu wa Pili ambae ni wa kike, hatukufuata "tarehe" maalum...
Post a Comment